Thursday 14 March 2013

Raila na CORD kuenda cortini kupinga maamuzi ya wa Kenya


MGOMBEA urais wa muungano wa CORD Raila Odinga amesema atapinga ushindi wa Uhuru Kenyatta wa Jubilee kortini. Amesema kuna makosa mengi katika ujumlishaji wa kura na kutoa wito kwa wafuasi wake wawe watulivu na kudumisha amani anapotafuta usaidizi Mahakama ya Juu.









MGOMBEA urais wa muungano wa CORD Raila Odinga amesema atapinga ushindi wa Uhuru Kenyatta wa Jubilee kortini. Amesema kuna makosa mengi katika ujumlishaji wa kura na kutoa wito kwa wafuasi wake wawe watulivu na kudumisha amani anapotafuta usaidizi Mahakama ya Juu.


Bw Kenyatta alipata kura 6,173,433 kati ya jumla ya kura 12,338,667 zilizopigwa katika uchaguzi huo wa Jumatatu ambazo ni asilimia 50.03 ya kura.
Bw Odinga aliibuka wa pili na kura 5,340,546 ambazo ni asilimia 43.28  ya kura zilizopigwa.

Alhamisi, muungano wa Coalition for Reforms and Democracy (Cord) ulikuwa umeitisha kusimamishwa kwa uhesabu wa kura ukisema shughuli hiyo ilikuwa ya kutiliwa shaka.
Kalonzo Musyoka, aliyekuwa mgombea mwenza wa Raila Odinga, alisema Tume Huru ya Muda ya Uchaguzi (IEBC) inafaa kulaumiwa.

No comments:

Post a Comment

Ji husishe kwa maoni yako ndio ukweli upatikane kwa manufaa wetu